Pages

Monday, December 19, 2011

UONGOZI WETU NA HATIMA YA TANZANIA-MWL NYERERE

Nchi yetu bado changa. Tusione haya kuendeleza taratibu ambazo zinaonekana kuwa zinafaa, na wala
kubadili zile ambazo japokuwa huko nyuma zimetufaa, lakini sasa "zimepitwa na wakati." Ndivyo
tulivyofanya kuhusu mfumo wa chama kimoja; tusiogope kufanya hivyo kuhusu mageuzi ya kuleta
demokrasia zaidi ndani ya Chama Cha Mapinduzi.
Inawezekana kwamba demokrasia peke yake ambayo kwa sasa itaendelea kuwa na maana kwa nchi hii
wakati tunasubiri kupata mpinzani mzuri na makini nje ya CCM, ni demokrasia ndani ya CCM.
Wanachama wa CCM wana wajibu wa kukitazama upya chama chao na kuona jinsi ya kuongeza
demokrasia ndani yake. Wajibu huu si kwa chama chao tu, ni wajibu wa uzalendo kwa manufaa ya
Tanzania nzima.
75
WOSIA
Ole wake Tanzania
Tusipoisaidia!
Niwezalo nimefanya:
Kushauri na kuonya.
Nimeonya: Tahadhari!
Nimetoa ushauri:
Nimeshatoka kitini;
Zaidi nifanye nini.
Namlilia Jalia
Atumulikie njia;
Tanzania ailinde,
Waovu wasiivunde.
Nasi tumsaidie
Yote tusiyamwachie!
Amina, tena Amina!
Amina tena na tena!
T A M A T I

No comments:

Post a Comment